|
SWALI: Nini hukumu ya udhu kwa mwanamke aliye zitia kucha zake hiki kinacho itwa leo "rangi ya kucha"?
JIBU: Hakujuzu kwa mwanamke anaye swali kupaka rangi kucha zake ikiwa rangi hiyo inayazuia maji kukufikia kiungo wakati wa kuchukua twahara ya udhu au josho. Na kila kitu kinacho zuia maji kufika kwenye kiungo kinacho twaharishwa, hakijuzu kutumiwa na mwenye kutawadha au mwenye kuoga, kwa sababu Allah Ataadhamiaye anasema: "...BASI OSHENI NYUSO ZENU, NA MIKONO YENU..." [05:06]
Na mwanamke akiwa amezipaka rangi kucha zake, bila ya shaka rangi hiyo inayazuia maji kukifikia kiungo kinacho oshwa, kwa ajili hiyo basi anakuwa bado hajauosha mkono wake. Na kwa kitendo chake hicho cha kutokukamilisha kuosha kiungo cha udhu, anakuwa ameiacha mojawapo ya nguzo za udhu/josho.
Allah ndiye Mjuzi mno. |