Search the web
Sign In
New User? Sign Up
Wanazuoni · Tanzania's Intellectuals

Group Information

  • Members: 416
  • Category: Tanzania
  • Founded: Aug 3, 2007
  • Language: English
? Already a member? Sign in to Yahoo!

Yahoo! Groups Tips

Did you know...
Real people. Real stories. See how Yahoo! Groups impacts members worldwide.

Messages

  Messages Help
Advanced
Mwanazuoni Evaristo Haulle AMATHUBUTU AMWEZA- HONGERA   Message List  
Reply Message #13461 of 14092 |
Enyi wanazuoni weledi,
Amani iwe nanyi

Napenda kumpongeza jukwaani mwanazuoni Evaristo Haulle kwa 'kukataa kufa'.
Amekataa kufa kwa kutoenda kuuza mchicha ama kuanzisha dirisha la kuuza sabuni pale nyumbani kwake, aitwe mjasiriamali.
Amekataa kufa kwa kugomea kunyamaa afe kibudu;
Amekataa kufa kwa kukionea haya Kiswahili lugha adhimu ya Taifa;
Mwenzetu kakataa kufa, amechapisha Diwani yake ya kwanza; ULIZA TU (kitabu cha mashairi),
amekataa kufa, amekibinua kiulizo!

Onja Ladha ya yaliyomo:
MAHABA
Mahaba ni kama moto, joto utafurahia
Mahaba ni kama moto, chakula utapikia
Mahaba ni kama moto, mwanga tajipatia
Mahaba ni kama moto pia unaangamiza,

Mahaba ni kama maji, mwilio wahitajia
Mahaba ni kama maji, kiu yatakukatia
Mahaba ni kama majiukikosa wajutia
Mahaba ni kama maji, yazoa yaangamiza

KAMA KWELI WAFAA:
Kama kweli unafaa, khanga vitenge vya nini?
Kama kweli unafaa,huhitaji bilioni
Kama kweli unafaa, huna haja kurubuni
Kama kweli unafaa, waonekana machoni.....

Na
WAFALME MWITUNI
Tembo na miguvu yako, ni vipi unatishika
Ndani ya himaya yako, kichwani unajishika
Tazama unyayo wako, sisimizi watishika
Ni nini uoga wako, waache waandamane.

Langu ni neno la pongezi kwako mwanazuoni Evaristo, changamoto umenipa.
Ninazo nakala chache kwa walioko Dar waweza kujipatia.

Adam


2 of 2 Photo(s)

Fri Jan 13, 2012 12:16 pm

lingsadam
Offline Offline
Send Email Send Email

Message #13461 of 14092 |
Expand Messages Author Sort by Date

Enyi wanazuoni weledi, Amani iwe nanyi Napenda kumpongeza jukwaani mwanazuoni Evaristo Haulle kwa 'kukataa kufa'. Amekataa kufa kwa kutoenda kuuza mchicha ama...
lingson adam
lingsadam Offline Send Email
Jan 13, 2012
12:16 pm

Pongezi za dhati kwa Mwanazuoni Kamaradi Evaristo! Adam, tuna shauku ya kusoma "tunu" hii, tunaweza kukupataje ili kujipatia nakala? Mathew Agripinus Senga, ...
Mathew Senga
magripinus Offline Send Email
Jan 13, 2012
1:15 pm

Evaristo UDALIKHE! Adamu, copy yangu niwekee pembeni kabisaaaa. 2012/1/13 Mathew Senga <magripinus@...>...
Atuwene Mbelle
atuwene.mbelle@... Send Email
Jan 13, 2012
1:19 pm

Dada wa mimi Atu, unao uhakika utaipata nakala yako. ________________________________ From: Atuwene Mbelle <atuwene.mbelle@...> To:...
lingson adam
lingsadam Offline Send Email
Jan 13, 2012
1:21 pm

Vema Mathew, Kwa wewe naweza kukupitishia hapo kijiweni kwako, au ukipita kijiweni kwangu utakipata. Ahsante. ________________________________ From: Mathew...
lingson adam
lingsadam Offline Send Email
Jan 13, 2012
1:19 pm

Nitashukuru sana Kamaradi ukiweza kunipitishia kijiweni kwangu. Ahsante sana! Mathew Agripinus Senga, Assistant Lecturer, Department of Sociology and...
Mathew Senga
magripinus Offline Send Email
Jan 13, 2012
1:22 pm

Haluuuuuu.....Aise Adam pitishia mimi hiyo kitu pale Hillpark kama sio leo hata kesho mkuu! na sasa baada ya kupamba si tusherehekeeee.....Haule wapi papa...
bernard baha
bahabp2003 Online Now Send Email
Jan 13, 2012
1:36 pm

Kamaradi Bernard, Umepataaaaaaaaaa. au nkukute pale kwa nyani wetu kule kwenye kambi ya efu efu yuuuu siku hizi?? ________________________________ From:...
lingson adam
lingsadam Offline Send Email
Jan 13, 2012
1:39 pm

Haluuu ile sehemu sasa sio full kujiachia kama enzi zile,waweza kaa na mwenzio meza jirani ukidhania mteja kama weye kumbe mwenzio yupo kazini kudhibiti...
bernard baha
bahabp2003 Online Now Send Email
Jan 13, 2012
1:45 pm

Hakika nimeuona weledi wake kaka Haule. Hongera sana. Nami nitajitafutia kopi yangu ya kitabu chake. Aksante Adamu kutujuza haya. Sulle...
Emmanuel Sulle
esulle46@... Send Email
Jan 13, 2012
6:35 pm

Mie nishakamata kopi yangu loooooong tym! naanza kuufaidi uhondo ndani ya ULIZA TU! ________________________________ From: Emmanuel Sulle <esulle46@...> ...
bernard baha
bahabp2003 Online Now Send Email
Jan 14, 2012
7:17 am
Advanced

Copyright © 2010 Yahoo! Inc. All rights reserved.
Privacy Policy - Terms of Service - Guidelines NEW - Help