|
Ndugu wanazuoni,
Kwanza kabisa niwapongezeni wote kwa kukubali wazo hili lakuwa na
baraza la mazungumzo kwa njia hii,ndg Mtango anastahili pongezi za
pekee kwa kuwezesha huu utaratibu na amekuwa mwanademokrasia wa
kutushirikisha katika uchaguzi wa jina la kikundi. Wito wangu kwenu
ni kujitahidi kupitia katika mtandao wetu huu na kushiriki kikamilifu
katika mijadala inayoendelea pamoja na kuibua mijadala mipya pale
inapobidi. Bila shaka pamoja na ujana wetu tayari tunauzoefu wa
kutosha katika masuala mbalimbali ya nchi yetu.
Juzi nilihudhuria GDSS pae TGNP na kulikuwa na mada juu ya
uwajibikaji wa wabunge na bunge letu kwa ujumla kwa wananchi.
Mapungufu yaliainishwa ya kanuni mablimbali za Bunge zinazowanyima
uhuru wabunge lakini pia kama kawaida ya wanasayansi ya Jamii
hatukuishia katika kuangalia kanuni tu,tuliendelea katika kuchambua
mfumo mzima wa Bunge letu na kwa ujumla tatizo la uwajibiaji kwa
wabunge wetu ni la kimfumo zaidi ya kanuni.Nitaendelea kuwajulisha
yaliyojili huko na mifano halisi iliyotokea jana bungeni ambapo
mheshimiwa Kabwe alikumbana na rungu la kanuni,na kuambiwa kwamba
kama hoja zake kuhusu EPA kazipata kutoka kwa Asasi za Kijamii hana
authority ya kuongelea zaidi ya Mawaziri!
tukae Mkao wa kula,
Mwenzenu,
Baha.
|